Kauli mbiu ya
maadhimisho ya siku hiyo mwaka 2018 ni Redio na Michezo.
Maadhimisho ya siku
ya Redio Duniani nchini Tanzania yanadhimishwa kitaifa Mkoani Dodoma.
Kauli mbiu ya siku
hiyo inalenga kukuza michezo kwa kuzingatia jinsia kupitia Redio.
Maadhimisho hayo
yametanguliwa na mafunzo ya waandishi wa habari wa Redio za Jamii nchini
Tanzania kuhusu uandaaji wa habari na Vipindi bora, Jinsia na uandishi wa
habari za uchunguzi.
Akizungumza na washiriki
wa mafunzo hayo, Mkuu wa Ofisi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi
na Utamaduni, UNESCO, Bi Faith Shayo amewataka waandishi wa habari kuandika
habari sahihi na zenye tija kwa jamii.
Mafunzo hayo
yameshirikisha waandishi wa habari 49 kutoka vyombo vya habari 24 nchini na
yamefadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni,
UNESCO.
No comments
Post a Comment