WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI WATAKIWA KUTOINGILIA UHURU WA WANAHABARI

Wamiliki wa vyombo vya habari nchini wametakiwa kutoingilia uhuru wa wanahabari katika vituo vyao kwa sababu vinaongozwa na sera na misingi ya taaluma ya habari.
Hayo yamebainishwa     mjini DODOMA na Mkufunzi Mwandamizi wa  Radio za kijamii Bi Rose  Mwalimu katika warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari vijijini ambayo imewakutanisha wadau wa Redio za jamii nchini.
Amesema ni vyema wanahabari wakawa huru katika kutimiza wajibu wao kitaaluma ili kuihudumia jamii na kujiepusha na  masuala binafsi.
Warsha hiyo ya siku nane imewashirikisha wadau wa Redio za jamii 24 imeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO ili kuwajengea uwezo waandishi wa habari kujiendesha kwa kujiamini.


TAG