Shirika
la Kimataifa la Save the Children
kwa kushirikiana na shirika la Rafiki
Social Development Organization (SDO)mjini Shinyanga wamefanya mkutano wa ‘Klabu za Tuseme’ kutoka shule 8 za
msingi na sekondari kwa ajili ya kufanya tathmini juu ya klabu hizo katika
kupiga vita ukatili dhidi ya watoto.
Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Empire Hotel Mjini Shinyanga na kukutanisha wanafunzi kutoka shule 8 za msingi na sekondari ambazo ni Ushirika,Mwasele,Solwa,BugoyiA,Lyabusalu,Masekelo, Iselamagazi na Mwantin katika manispaa ya shinyanga na halmashauri ya shinyanga vijijini.
Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Empire Hotel Mjini Shinyanga na kukutanisha wanafunzi kutoka shule 8 za msingi na sekondari ambazo ni Ushirika,Mwasele,Solwa,BugoyiA,Lyabusalu,Masekelo, Iselamagazi na Mwantin katika manispaa ya shinyanga na halmashauri ya shinyanga vijijini.
Mratibu
wa Ulinzi wa mtoto,haki za watoto na utawala kutoka Shirika la Save The Children Alex Enock amesema
klabu za Tuseme zimeundwa kupitia mradi wa ulinzi wa mtoto,haki na utawala
unaotekelezwa na shirika hilo kwa kushirikiana na Shirika la Rafiki SDO kwa
ufadhili wa shirika la Maendeleo la nchini Sweeden (SIDA).
Enock amesema lengo la klabu hizo
ni kumsaidia mtoto wa kike kukabiliana na vitendo vya ukatili ikiwemo kupewa
ujauzito na kuepuka vishawishi mbalimbali ili aweze kumaliza masomo yake
salama.
Naye
afisa mradi wa ulinzi wa mtoto,haki na utawala kutoka Shirika la Rafiki SDO,Tangi Clement ameeleza
katika kutekeleza mradi huo wameshirikiana na idara ya elimu msingi na
sekondari kuanzisha klabu za Tuseme kwa ajili ya kuhamasisha ufaulu hasa kwa
watoto wa kike.
Wakizungumza
katika mkutano huo,wanafunzi hao wamesema klabu hizo zimewasaidia kwa kiasi
kikubwa kujiamini,kuepuka vishawishi mbalimbali lakini pia wamekuwa mabalozi
wazuri katika kuielemisha jamii juu ya haki za watoto.
No comments
Post a Comment