TATIZO LA MAJI KUWA HISTORIA , MSALALA KAHAMA.




Image result for MRADI WA MAJI SHINYANGA Mikoa miwiliya Shinyanga na Geita  imetiliana saini na kampuni ya ukandarasi ya kutoka China ya Beijing Construction Engeneering Group kwa ajili ya utekekelezaji wa mradi wa maji unaoanza mapema mwezi  januari mwakani.
Akizungumza kabla ya utiliaji wa saini hiyo ya makubaliano kati ya tanzania na china mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhil Nkurlu kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa shinyanga,amesema mradi huo mkubwa wa maji utakuwa na manufaa kwa wananchi wa halmashauri ya Msalala, Shinyanga vijijini  na Nyangh'wale mkoani Geita .
Aidha amewataka wakandarasi hao kukamilisha mradi huo kwa wakati ama kabla ya muda uliopangwa ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kuondokana na adha ya maji ya muda mrefu.
Mara baada ya utiliaji wa saini ulio wekwa na mkurugenzi wa msalala simon berege na mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi Cheng Long Hai ambapo kwa pamoja wamekamilisha zoezi hilo ili kuanza kwa mradi huo.
Akizungumza mara baada ya zoezi hilo mbunge wa jimbo la msalala  Ezekiel Maige amesema mradi huo umekuwa ni chachu na tumaini jipya kwa wananchi wa jimbo lake kwani watu wamekuwa wakipata shida ya maji bila ufumbuzi kwa muda mrefu.
Mradi huo unatarajia  kughalimu shilingi bilioni 13.9, na utatekelezwa kwa miezi kumi na mbili na utakamilika mapema desemba 6 mwakani .



TAG