RAIS MAGUFULI AMTOA BABU SEYA GEREZANI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasamehe familia ya mwanamuziki Pappi Nguza Viking ambao walikuwa wamehukumiwa kifungo cha maisha.
Rais Magufuli ametangaza msamaha huo leo mjini Dodoma kwenye sherehe za Uhuru wa miaka 56 ya Tanganyika, ambapo pia ametoa msamaha kwa wafungwa 8,157.
“Nimeamua kusamehe wafungwa 8157, ambapo baada ya msamaha huu, 1828 watatoka leo, 6329 wamepunguziwa muda wa kukaa gerezani”, amesema Rais Magufuli.
Baada ya kutangaza hivyo rais Magufuli akaongeza kuwa katika msahama huu nimeamua kuisamehe familia ya Nguza Viking na kuanzia sasa wawe huru kulingana na taratibu za kimagereza.
Nguza na wanawe watatu walikamatwa Oktoba 12 mwaka 2003 na walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Oktoba 16, mwaka 2003, wakituhumiwa kubaka na kunajisi watoto 10, na Juni 25, 2004 Mahakama iliwatia hatiani na kuwahukumu kwenda jela maisha kwenye Gereza la Ukonga, Dar es Salaam

TAG