KUHUDHURIA KLINIKI NI MKOMBOZI KWA MJAMZITO, KAHAMA.









Image result for WAJAWAZITO KUHUDHURIA KLINIKI

Wanawake wajawazito wameshauriwa kujenga tabia ya kuhudhuria kliniki pale wanapopata ujauzito ili kuepuka madhara mbalimbali wanayoweza  kuyapata ikiwemo  kifafa cha mimba.
 Ushauri huo umetolewa leo na dokta Frola Mwinuka kutoka halmashauri ya mji wa kahama wakati akizungumza katika kipindi cha nondo kinachorushwa kuanzia jumatatu hadi alhamis kupitia Baloha Fm
Amesema baadhi ya wanawake wamekuwa wazembe kuhudhuria kliniki mpaka pale wanapo karibia kujifungua  na wasichana wanao beba mimba katika umri mdogo na hivyo kujiweka katika hatari kubwa ya kupata kifafa cha mimba.
Dokta Mwinuka pia amebainisha madhara ambayo anaweza kupata mwanamke endapo atapata kifafa cha mimba na kusisitiza watu wakaribu na mama mjamzito kuhakikisha wanamuhimiza kuhudhuria kliniki.
Aidha amesisitiza jamii kutokimbilia dawa za kienyeji kutibu tatizo hilo ama mama kujifungulia nyumbani na badala yake wamuwahishe katika kituo cha kutolea huduma za afya.
TAG