
Imeelezwa kuwa mfugaji asiyeshiriki katika zoezi la
upigaji chapa hataruhusiwa kuuza ama kusafirisha mifugo yake katika Halmashauri ya mji wa Kahama wilayani humo
mkoani Shinyanga.
Akizungumza na Baloha fm Afisa Mifugo na Uvuvi wa
Halmashauri ya mji wa Kahama Costantine Lugendo amesema zoezi hilo ni
muhimu kwa mfugaji na ni agizo la
serikali kuu na linafanyika nchi nzima.
Aidha
Lugendo ameiambia Baloha FM kuwa
zoezi hilo lina manufaa kwa mfugaji kwani litawezesha utambuzi wa mifugo endapo
imepotea.
Hata
hivyo Afisa Mifugo huyo amebainisha kuwa zoezi la upigaji chapa lilianza mapema
mwezi Machi mwaka huu lakini lilisimama baada ya kuwepo na changamoto ya nyenzo
za kufanyia kazi.
Zoezi
la upigaji chapa amefafanua ni endelevu
ambapo litakuwa linafanyika mara baada ya miezi kadhaa huku umri wa ng'ombe
kuwekewa chapa ni kuanzia umri wa miezi 6.
No comments
Post a Comment