Kufuatia kuanza siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia jamii
imehimizwa kushiriki kupinga vitendo vyote vya kikatili.
Hayo yamesemwa na mkuu wa kitengo cha
dawati la jinsia Polisi wilayani Kahama mkoani Shinyanga NINAELI KISAGASE wakati akizungumza na Baloha
fm.
KISAGASE
amesema endapo jamii itashiriki kikamilifu kupaza sauti kutoa taarifa itasaidia
watuhumiwa kukamatwa na sheria kuchukua mkondo wake.
Amesema licha ya ukatili wa kijinsia
kuendelea lakini jamii imeanza kupata uelewa kuhusu haki zao za msingi pale zinapovunjwa na kutoa maelezo katika
dawati hilo.
Aidha ameeleza kwa sasa wapo katika siku kumi na sita za
kupinga ukatili hivyo jamii haina budi kutoa
taarifa kwa haraka na sio kuyafumbia macho pindi wanapoona matendo ya kikatili
yakitendeka.
No comments
Post a Comment