JKT RUVU YAINGIA KAMBINI

Image result for jkt ruvu
Timu ya soka ya JKT RUVU inayoshiriki ligi daraja la Kwanza imeingia kambini ili kujifua zaidi kwa ajili ya michezo iliyosalia ya ligi hiyo.

JKT RUVU iko kundi A katika ligi hiyo.

Afisa Habari wa Timu hiyo, COSTANTINE MASANJA ameiambia BALOHA FM kuwa JKT RUVU imeingia kambini chini ya Kocha Mkuu, BAKARI SHIME.

MASANJA amesema hatua hiyo inalenga kuiweka timu hiyo katika mazingira bora ikiwa ni kujiandaa kwa michezo ya ligi hiyo ambayo imebaki.

Kwa mujibu wa Ratiba ya Kundi A, Desemba 16, mwaka huu JKT RUVU itacheza na KILUVYA UNITED katika uwanja wa FILBERT BAYI uliopo Mkoani PWANI.

Katika hatua nyingine, Timu ya JKT RUVU haikufanya mabadiliko katika dirisha dogo la usajili.
TAG