Mataifa 10 yatashiriki katika michuano hiyo na tayari
droo ya hatua ya makundi imeshatangaza.
Kundi A lina timu za KENYA, RWANDA, LIBYA, TANZANIA na ZANZIBAR
wakati Kundi B litakuwa na mataifa ya UGANDA, ZIMBABWE, BURUNDI, ETHIOPIA na SUDAN
KUSINI.
Mechi ya ufunguzi itakuwa kati ya wenyeji KENYA na RWANDA
lakini mechi nyingine siku hiyo ya kwanza itakuwa ni kati ya LIBYA na TANZANIA.
Michuano hiyo itachezwa katika uwanja wa Bukhungu mjini
Kakamega, Afraha Nakuru, Mumias Sports Complex na Moi, mjini Kisumu.
Hata hivyo, kuna wasiwasi michuano hii isifanyika MJINI
Kisumu kwa hofu za kiusalama kwa mujibu wa chama cha soka nchini Kenya na sasa
uwanja wa Machakos utatumiwa.
Katika Hatua nyingine, Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya ZANZIBAR
(ZANZIBAR Heroes), HEMED SULEIMAN ‘MOROCCO’ amemuongeza kwenye kikosi kiungo
mshambuliaji wa timu ya YANGA, EMANUEL MARTIN ili kuzidi kuipa nguvu timu hiyo
itakayokwenda Kenya katika Mashindano ya CECAFA yanayotarajiwa kuanza Desemba 3
hadi 17, 2017.
Katika uteuzi wa awali Martin hakuitwa lakini kocha Morocco
amelazimika kumuongeza mshambuliaji huyo na atakuwa mchezaji wa 31 kwenye
kikosi cha Heroes kabla ya kuchujwa na kubakia 24 ambao wanatarajia kuondoka
Zanzibar kesho Novemba 29, 2017.
Martin ambaye ni mchezaji wa zamani wa JKU ya Zanzibar
ataungana na wenzake Ahmed Ali (Taifa ya Jang’ombe), Nassor Mrisho (Okapi),
Mohammed Abdulrahman (JKU), Abdallah Haji ‘Ninja’ (Yanga), Mohd Othman Mmanga
(Polisi), Ibrahimm Mohammed ‘Sangula’ (Jang’ombe Boys), Adeyum Saleh ‘Machupa’
(Kagera Sugar), Haji Mwinyi Ngwali (Yanga), Abubakar Ame ‘Luiz’ (Mlandege),
Issa Haidar ‘Mwalala’ (JKU), Abdulla Kheir ‘Sebo’ (Azam) na Ibrahim Abdallah
(Taifa ya Jang’ombe).
Wengine ni Abdul-swamad Kassim (Miembeni City), Abdul
Aziz Makame (Taifa ya Jang’ombe),Mudathir Yahya (Singida United), Omar Juma
(Chipukizi), Mohd Issa ‘Banka’ (Mtibwa Sugar), Amour Suleiman (JKU), Mbarouk
Marshed (Super Falcon), Hamad Mshamata (Chuoni), Suleiman Kassim ‘Selembe’
(Majimaji), Kassim Suleiman (Prisons), Matheo Antony (Yanga), Ali Badru (Taifa
ya Jang’ombe), Feisal Salum (JKU), Salum Songoro (KVZ), Khamis Mussa (Jang’ombe
boys), Mwalimu Mohd (Jamhuri), Seif Abdallah ‘Karihe’ (Lipuli) na Ibrahim Hamad
Hilika (Zimamoto).
No comments
Post a Comment