SERIKALI YASHAURIWA KUANZISHA SOMO LA UKIMWI-SHULE ZA SECONDARI.



Serikali  kupitia Wizara ya Elimu  Sayansi na Teknolojia imeshauriwa  kuanzisha somo la Ukimwi katika shule za Sekondari,  ili kuwasaidia wanafunzi  kuepukana na  ugonjwa huo.

Hayo yamebainishwa na Diwani wa kata ya Ikinda Matrida Musoma ,wakati  akichangia taarifa ya utekelezaji  wa mradi wa kudhibiti Ukimwi  kwenye  kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Msalala kilichofanyika  mwishoni mwa wiki iliyopita.

Amesema taarifa hiyo  imebainisha kutekeleza  mradi huo kwa kuwapatia elimu  vijana  ambao  hawapo masomoni  huku kundi la wanafunzi wa shule za sekondari  likisahaulika.

Kutokana na hali hiyo serikali  inatakiwa  kuanzisha somo la ukimwi   katika shule za sekondari  ili elimu  hiyo  iwafikie  pia  wanafunzi  hao.

TAG