UKATILI WASABABISHA MAMA LISHE KUACHA VYAKULA NA KUANDAMANA, KAHAMA



 Image result for UKATILI WA KIJINSIA
Umoja wa Mama Lishe katika hospitali ya wilaya ya Kahama ,mkoani Shinyanga wameandamana mpaka kituo cha Polisi Kitengo cha Dawati la Jinsia Kahama kupinga kitendo cha Mama Lishe mwenzao   anayedaiwa kumfanyia ukatili wa kumpiga kichwani mtoto wa binamu yake  na kumsababishia majeraha.

Wakizungumza na Baloha FM  baadhi ya Mama Lishe hao wamemtaja mama huyo kuwa ni Veronica Ugwang'a mwenye umri wa miaka  (40)  anadaiwa kumpiga mtoto mwenye umri wa miaka  (9)  jina limehifadhiwa

Kwa upande wake Mwanamke  huyo aliyefanya ukatili huo alipohojiwa   amekiri kutenda ukatili   huo kwa madai  kuwa mtoto huyo amekuwa akijisaidia  kitandani mara kwa mara.

Naye Afisa Kitengo cha Dawati la Jinsia  wilayani Kahama Coplo.Methusela Gumba ameelezea kuhusiana na tukio hilo huku akiwataka watu kutoa ushirikiano ili kufichua ukatili katika jamii.

Kitendo hicho cha kikatili kinatajwa kufanyika katika mfululizo wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia maadhimisho ambayo hufanyika  Novemba 25 mpaka Disemba 10 ya kila mwaka.
TAG