ELIMU YA MAZINGIRA NI HAZINA KWA WATOTO, KAHAMA.



Image result for WANAFUNZI WAKIPANDA MITI
Imeelezwa kuwa tabia ya kuwajengea uwezo watoto katika kutunza mazingira,ni moja kati ya hazina kubwa kwa taifa itakayo saidia kutunza uoto wa asili .
Hayo yamebainishwa na mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Kahama B CONRAD NKUBA,iliyopo halmashauri ya mji wa Kahama wilayani Kahama mkoani Shinyanga, wakati akizungumza na Baloha fm ofsini kwake.
Amesema kwa kulitambua hilo shule hiyo imekuwa ikiwafundisha watoto hao suala la mazingira kikamilifu ikiwa ni pamoja na kupanda miti mbali mbali ili kuboresha mazingira ya shule.
Aidha amesema shule hiyo tayari imepokea miti 140 ya matunda aina ya miembe kutoka halmashauri ili kuweza kupanda na kuongeza kuwa kufikia mwaka 2018 shule hiyo itahakikisha inaweka uzio wa miti itakayo pandwa kuzunguka shule ili kuepuka  uvamizi wa watu.
Nkuba ameongeza kuwa shule hiyo ya Kahama B mbali na kupokea miti pia imekuwa na utaratibu wa kununua miti aina ya midodoma kila mwezi ili kuboresha mazingira ya shule na kupata kivuli kwa wanafunzi .
TAG