MAZINGIRA YA ENEO YAWA MKOMBOZI KWA ZAO LA KOROSHO USHETU

Image result for ZAO LA KOROSHO


Halmashauri ya  Ushetu   wilayani Kahama Mkoani Shinyanga, imeanzisha kilimo cha Korosho ili kutekeleza azima ya serikali ya  kuwa na mazao mkakati.
Mkurugenzi  Mtendaji    Michael Matomola amesema hayo katika uzinduzi wa kilimo cha zao hilo uliofanyika katika ofisi za Halmashauri hiyo.
 Amesema  wamedhamiria kutii wito wa serikali kupitia agizo lililotolewa na Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa la kuwa na mazao mkakati, ambapo wameamua kulima korosho  kutokana na mazingira ya eneo hilo.
Fortunus   Kapinga   ni  Mtafiti wa korosho  kanda ya Kusini ambapo amekili eneo hilo linafaa kwa kilimo hicho  huku akibainisha  mahitaji yanayotakiwa  ili kustawi  vizuri.
Anna Ngongi na Paul Senni ni Maafisa kilimo wa Halmashauri hiyo wamesema wakulima wameitikia  kilimo hicho kupitia uhamashaji uliofanywa na viongozi wao wakiwemo Madiwani.
Halmashauri ya Ushetu mpaka sasa imepokea kiasi cha kilo 80 za mbegu   kutoka bodi ya korosho Tanzania, na  kuzisambaza kwa  kata  ya Mapamba na Nyamilangano hu kukiwa bado  kuna uhitaji  kwa maeneo mengine.
 
TAG