MABISHANO YA ENEO LA KUJENGA MAKAO MAKUU YAWATOKEA PUANI- MSALALA.


Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga imeagizwa  kuhamia eneo la Ntobo kabla ya   Juni 30  ,mwaka 2018.
Agizo hilo limetolewa na Naibu waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Joseph George Kakunda katika  hafla ya makabidhiano ya majengo yaliyokuwa yanatumiwa na halmashauri ya Ushetu na kuyakabidhiwa halmashauri ya mji wa Kahama baada ya Halmashauri hiyo ya Ushetu kujenga majengo yao eneo la Nyamilangano.

Naibu waziri huyo wa TAMISEMI amesema kuwa mabishano ya  kuamua makao makuu ya halmashauri  ya Msalala serikali haihusiki hivyo ni matatizo ya ndani ya halmashauri hiyo.

Aidha Naibu waziri huyo amesema kuwa tamko hilo litatolewa kwenye maandiko ndani ya siku 10 huku akiitaka halmashauri hiyo kubeba jukumu la kuhamia Ntobo.

Imeelezwa kuwa Halmashauri ya Msalala imechelewa kuhamisha ofisi  zake katika eneo lake baada ya kuwepo mgongano wapi makao makuu ya halmashauri hiyo yawekwe kati ya Segese na Ntobo na hatimaye wamekubaliana makao makuu kuwa eneo la  Ntobo.
TAG