MTI KWANZA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI, KAHAMA.

Image result for upandaji miti
Wananchi wilayani kahama wametakiwa kupanda miti kwa  kuzitumia mvua zinazoendelea kunyesha ili kukabiliana na mabadiliko ya  tabia  nchi. 
Kauli hiyo imetolewa na baadhi ya wananchi mjini kahama wakati wakizungumza na baloha fm kuhusu kampeni ya upandaji wa miti iliyoanzishwa mkoani humo ya shinyanga mpya mti kwanza.
Wamesema licha ya mvua zinazoendelea kunyesha wananchi hawana destri ya kupanda miti ingawa serikali imekuwa ikihimiza wananchi wote kupanda miti  hiyo.

Kwa upande wake meneja msaidizi wa wakala wa misitu Tanzania wilaya ya kahama MOHAMED DOSA amewataka wananchi kupanda miti kwa kuwa kuna mabadiliko makubwa yaliyotokana na kutoweka kwa miti.

Hata hivyo amesema mpaka sasa taasisi hiyo ya wakala wa misitu kahama imeotesha miti laki tano kwa ajali ya kupandwa katika maeneo mbalimbali ya mji wa kahama katika taasisi za umma.
TAG