WASANII KAHAMA WAUNDA UMOJA.



Vijana wanaofanya kazi ya sanaa ya muziki katika Wilaya ya KAHAMA mkoani SHINYANGA wameamua kuunda umoja wao ambao utawatambulisha ndani na nje ya wilaya hiyo.
Mwenyekiti wa Umoja huo wilaya ya KAHAMA, AGUSTINO MALYA amesema hayo wakati akizungumza na BALOHA FM.
MALYA amesema wameamua kuunda umoja huo ambao utatambulika kwa jina la Golden city Arts unity lengo likiwa ni kusaidiana wao kama vijana pamoja na kuendeleza na kukuza sanaa ya muziki ndani na nje ya KAHAMA.
Aidha Ameongeza kuwa wamelenga kufikisha ujumbe katika jamii kupitia sanaa ya muziki ikiwemo kupinga mauaji ya vikongwe na watu wenye Ualbino na mambo mengine yanayoenda kinyume na maadili ya Kitanzania
Kwa upande wao, baadhi ya wasanii ambao wameshiriki kuunda umoja huo wamesema utawasaidia kufikia malengo yao kwani sanaa ni kazi kama kazi zingine.
Kadhalika wamewataka wazazi wenye watoto ambao wanavipaji kuwapa uhuru wa kufanya sanaa.




TAG