BALE YUKO FITI - ZIDANE



Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amesema Mshambuliaji wa timu hiyo, Gareth Bale amepona na yuko fiti kurejea uwanjani.
Bale atacheza kwa mara ya kwanza leo baada ya kukaa nje kwa miezi miwili.
Kocha Zidane amesema madaktari wamethibitisha kuwa Bale amepona na yupo tayari kukabili wapinzani wao katika michuano mbalimbali inayoshiriki timu hiyo.
Amefafanua kuwa Mshambuliaji huyo ataongeza nguvu katika kikosi cha Real Madrid.
Bale amekuwa nje ya dimba baada ya kupata na majeraha ya goti na baadae nyonga na kwa sasa amejumuishwa katika timu itakayocheza na Fuenlebrada kwenye kombe la Copa del Rey.
Bale raia wa Wales alionekana mara ya mwisho uwanjani walipoichapa Borussia Dortmund 3-1 kwenye kombe la klabu bingwa Ulaya.
Amefunga jumla ya magoli 70 katika michezo 159 aliyoichezea Real Madrid.


TAG