WANAFUNZI WAHAMIA SHULE JIRANI SABABU YA CHOO, KAHAMA



Ukosefu wa vyoo katika shule ya msingi  kahama A wilayani kahama mkoani shinyanga  umesababisha wanafunzi wa shule hiyo kutumia vyoo vya shule ya jirani Kahama B.



Akizungumza na baloha fm diwani wa kata ya kahama mjini Hamidu Kapama amesema kuwa  choo cha awali kimetitia na hivyo kubomoka hali inayoweza kusababisha milipuko ya magonjwa hasa kipindi hiki cha masika.



Amesema kuwa baada ya  tukio hilo ameweza kuitisha mkutano na wazazi lengo ikiwa ni kuchangia ujenzi wa vyoo bora katika shule hiyo.



Kutokana na kikao hicho wazazi na walezi wameonyesha ushiriki mzuri kwa kuahii kuunga juhudi za Rais Magufuli kwa kuahidi kuchangi mifuko ya saruji.



Aidhaa amesema kuwa lengo lao ni kujenga choo chenye matundu 12  ili wanafunzi waweze kupata mahali pa kujisitiri na tathimini ya ujenzi huo inatarajia kughalimu zaidi ya shilingi milioni 10.
TAG