TATIZO LA MAJI LASHUSHA UFAULU MSALALA.

Imeelezwa kuwa chanzo cha kupata matokeo  mabaya ya ufaulu, baadhi ya  shule za msingi na Sekondari  katika halmashauri ya Msalala mkaoni Shinyanga,  ni kutokana na wanafunzi  na walimu kutumia muda mwingi kutafuata maji kwaajili ya matumzi ya shule.

Akizungumza leo katika kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo, Diwani wa Kata ya MWANASE, SAMSON MASANJA amesema shule nyingi hasa zilizo pembezoni zina changamoto ya upatikani wa huduma ya Maji.
Amesema kutokana na hali hiyo, wanafunzi na walimu hulazimika kutumia muda wa asubuhi kufuata  maji umbali mrefu kwaajili ya  matumizi ya shule hivyo kuathiri ratiba ya masomo darasani.


Masanja ameshauri Halmashauri hiyo kuja na mapango kabambe wa kukabiliana na hali hiyo ili kuwawezesha wanafunzi kufaulu mitihani yao.


Awali halmashauri hiyo imeeleza kua sababu zilizosababisha halmashauri hiyo kupata matokeo mabaya  kwa shule za Msingi na Sekondari ni kutokana na ukosefu wa Chakula Mashuleni, Utoro, ukosefu wa walimu   hasa wa masomu ya sayansi pamoja na mwamko duni wa wawazi.


Aidha  halmashauri hiyo kupitia Kitengo cha Elimu imesema imejipanga kuinua kiwango cha ufaulu mwaka huu.


Na Michael Francis Bundala.
TAG