KUPIGWA MNADA JENGO LA YANGA, MKWASA AWATOA WASIWASI WANAYANGA.





WIZARA ya Ardhi Maendeleo ya Makazi imetangaza kulipiga mnada jengo la klabu ya Yanga, makao makuu makutano ya mitano ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam kesho. 
Katika tangazo lililotoka leo, Wizara ya Ardhi imesema hatua hiyo inafuatia kesi iliyofunguliwa na Kamishna wa Ardhi katika Baraza la Ardhi na Nyumba Wilaya na Temeke na Ilala dhidi ya Yanga.
Na kwa mujibu wa tangazo la kampuni ya udalali ya Msolopa Investmenst Limited, Dalili Maurid Msolopa amesema mnada huo utafanyika hapo baadaye hapo hapo Jangwani, baada ya kushindikana hii leo.

Akizungumzia hilo, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa amesema kwamba ameshitushwa na tangazo hilo kwa kuwa tayari wapo katika jitihada za kulipa madeni yao.
 
Mkwasa
amesema kupitia utaratibu ambao wamejiwekea wanaamini utakuwa msaada wa kumaliza kulipia deni hilo.

 
Katika hatua nyingine Mkwasa amesikitishwa na kuwepo kwa hali hii wakati timu ikiwa kwenye maandalizi ya mchezo wa ngao ya Jamii shidi ya mahasimu wao Simba. 

TAG