TFF YATIA NGUMU UBADILISHWAJI WA RATIBA.



 TFF.
Shirikisho la soka nchini TFF limesimamia msimamo wake wa kuheshimu ratiba ya kuanza kwa msimu mpya wa 2018/17, licha ya kushauriwa kurudisha nyuma mchezo wa kuwani ngao ya jamii ambao utawakutanisha mahasimu wa soka la Bongo Wekundu wa Msimbazi Simba dhidi ya Young Africans.


Afisa habari wa shirikisho hilo Alfred Lucas amesema wanaheshimu mawazo na michango iliyowasilishwa TFF na wadau wa soka kuhusu mabadiliko ya mchezo huo, lakini akaeleza hawatobadilisha tarehe ambayo waliitangaza wakati wakitoa ratiba ya msimu mpya.



Zoezi la kuchukua fomu za kuwani nafasi za uongozi wa kamati ya bodi ya ligi zimeanza kwa kusuasua ikiwa ni siku ya kwanza ya mchakato wa kuelekea kwenye uchaguzi ambao utafanyika jijini Dar es salaam mwezi ujao.


Afisa habari wa shirikisho la soka nchini TFF Alfred Lucas amesema waliutarajia huenda viongozi wa klabu za ligi kuu na ligi daraja la kwanza wangejitokeza kwa wingi hii leo, lekini imekua tofauti.



Wakati huo huo wachezaji watatu waliokuwa kwenye timu ya soka ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, Ally Ng’anzi, Yohana Oscar Nkomola na Erick Nkosi wameondoka nchini Alfajiri ya leo kwenda Tunisia kwa ajili ya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa.


Serengeti Boys ikiundwa na vijana wenye vipaji kutoka mikoa tofauti, iliweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza ya vijana Tanzania kucheza Fainali za Afrika baada ya kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 mwezi Mei mwaka huu nchini Gabon. 


Na kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Cambiasso Sports Centre, Twaha Ngwambi, vijana hao wote wamepata mwaliko wa klabu ya Etoile du Sahel ya Ligi Kuu ya Tunisia.


Ngwambia amesema mwaliko huo unafuatia vijana hao wote kufanya vizuri wakiwa na timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 mwaka huu.



Ngwambia amesema kwamba Ng’anzi na Nkosi wanakwenda kufanya majaribio, wakati Nkomola anakwenda moja kwa moja kujiunga na akademy ya timu hiyo ambako atasaini mkataba.

Pamoja na kutolewa katika hatua ya makundi nchini Gabon, Serengeti Boys ilivutia kwa soka yake, huku vijana wengi wakitabiriwa kufika mbali zaidi kisoka.
TAG