MBUNGE USHETU AOMBWA KUTATUA CHANGAMOTO YA MIUNDOMBINU.




Wananchi wa kijiji cha Butende kata ya Mpunze halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga wamemuomba mbuge wa jimbo la Ushetu bw, Elias Kwandikwa kutatua changamoto ya barabara inayotoka mpunze kuelekea kijijini hapo ili kurahisisha shughuli za usafirishaji.


Kauli hiyo imetolewa na wananchi hao wakati wakizungungmza katika mkutano wa hadhara na mbunge huyo alipofanya ziara ya kutembelea kijiji hicho ili kujionea changamoto mbalimbali zinazowakabili.


Baadhi ya wananchi hao Daud Charles na Hamis Mnyole, wamesema ubovu wa barabara hiyo umekuwa ni changamoto kubwa ambayo husababisha madhara kwa watumiaji ikiwemo ajali za mara kwa mara kutokana na magari kushidwa kupita.


Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Ushetu Elias Kwandikwa  amesema kuwa serikali kupitia halmashauri hiyo imekwisha kuanza mikakati ya kutatua changamoto za barabara  na ameahidi kupeleka gari la kukwangua barabara ili zoezi hilo lianze mara moja.




Aidha Mbunge huyo amewaomba wananchi hao kuendelea kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano kwani serikali imekwisha wakala wa barabara TARULA kwa lengo la kushughulikia changamoto za barabara.
TAG