Hayo yamebainishwa leo na Daktari Frola Mwinuka kutoka Halmashauri ya Mji Kahama, wakati akiongea kwenye kipindi cha Darubini Halisi kinachorushwa na Baloha Fm.
Amesema ni vyema kujifungulia katika vituo vya afya ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza wakati wa kujifunga ikiwamo kupoteza maisha Mama na Mtoto anayezaliwa.
Aidha mesema takwimu za mwaka 2015 zinaonyesha kuwa wasichana mililoni 14 wanabeba mimba kila mwaka Duniani, huku Mkoa wa Shinyanga ukitajwa kuongoza nchini Tanzania ukifuatiwa na Mkoa wa Tabora.
Amesema chanzo ha mimba za utotoni ni umaskini katika familia, kukosa elimu ya afya uzazi, anasa, pamoja na ndoa za utotoni na kwamba mschana anayepata mimba chini ya umri huo anaweza akaathirika kimwili na za kisaikolojia.
Hata hivyo amesema ili kunusuru hali hiyo sheria ichukue mkondo wake kwa wale watakaokuwa visababishi, pia jamii ihamasishe wanawake wenye mimba kwenda kujifungulia hospitalini.
Na Mary Clemency Baloha fm.

No comments
Post a Comment