
Waziri wa mambo ya
ndani ya nchi Mwigulu Chemba ameliagiza Jeshi la polisi Mkoani
Shinyanga kuwachukulia hatua
madereva pikipiki na abiria ambao
hawavai kofia ngumu.
Akiwa ziarani Mkoani
Shinyanga hivi karibuni Waziri
Nchemba amesema kuna baadhi ya abiria wanakataa kuvaa kofia
ngumu kwakudai kuwa wanaharibu nywele zao
hali ambayo inahatarisha usalama
wao.
Aidha amesema Jeshi la polisi kitengo cha usalama
barabarani kinatakiwa kuwachukulia hatua kali wale watakaobainika kukiuka
sheria ya usalama barabarani.
Nao baadhi ya
wananchi wa wilaya
ya Kahama Emmanuel Sosoma,Sali
Bunzali na Robert Misungwi kupitia
kipindi cha Darubini Halisi cha Baloha Fm
wamepongeza agizo hilo
lililotolewa na serikali
kwakutoa mitazamo yao tofauti.
Na Mary Clemence Baloha FM Kahama.
No comments
Post a Comment