LHRC YAMTAKA KAIMU JAJI MKUU KUKEMEA UVAMIZI WA IMMMA ADVOCATES.



Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimemtaka Kaimu Jaji Mkuu, Ibrahim Juma kukemea hadharani shambulizi lililofanyika katika ofisi za wanasheria za Immma Advocates.

Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo-Bisimba amesema tangu kutokea mlipuko usiku wa kuamkia Agosti 26, hakuna kiongozi wa Serikali ambaye amekemea.

Amesema hata kaimu jaji mkuu anayesimamia mhimili wa Mahakama naye amekaa kimya kama vile hakuna tukio lililotokea.

Dk Kijo-Bisimba amesema leo Agosti 29 kuwa, kitendo cha mawakili kuvamiwa kimewatia hofu wanataaluma hao.

 Katika hatua nyingine Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika ‘TLS’, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameendelea kulaani tukio la kuvamiwa ofisi za Wanasheria IMMMA Advocates na kusema ni muhimu jambo hilo likapigiwa kelele kwa kuwa siyo la kisiasa.

Lisu amesema hayo baada ya kualikwa katika mkutano wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)na kusema kuna mashirika mengi yasiyokuwa ya kiserikali ndani ya Tanzania ambayo yanafanya kazi za kutetea haki za binadamu lakini wengi wao katika tukio hili wamekuwa wapo kimya.

2.Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dk Augustine Mahiga amesema kikundi chochote cha kigaidi au kiharamia kitakachoingia katika moja ya nchi zilizo katika ukanda wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) kitajuta.

Akizungumza  kwa sababu kikundi hicho cha uigaidi kitashambuliwa na majeshi ya nchi zote katika ukanda huo iwapo kitaanza uchokozi.

Amesema nchi za Sadc zimeamua kujizatiti katika ulinzi kwa kuunganisha majeshi yake ili kujiweka sawa na tishio lolote la ugaidi na uharamia zikiamini uchumi wake hautaimarika kama moja ya nchi itakuwa inasumbuliwa na ugaidi.

Balozi Mahiga amesema hayo wakati akifunga mazoezi ya pamoja ya kijeshi yaliyopewa jina la Ex-Matumbawe yaliyoendeshwa na majeshi kutoka nchi saba zilizo katika jumuiya ya Sadc yaliyofanyika mkoani Tanga na kuhitimishwa jana Agosti 28.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ), Jenerali Venance Mabeyo, amesema mazoezi ya Ex-Matumbawe yenye madhumuni ya kimkakati, utendaji kivita na ki-mbinu yamefanyika nchini kwa mara ya kwanza baada ya kuendeshwa Zambia, Lesotho, Afrika Kusini, Namibia, Angola na Zimbabwe.


TAG