ARSENAL 1-3 MANCHESTER UNITED


Image result for arsenal vs manchester utd



Manchester United imekuwa timu ya Kwanza kupata ushindi katika uwanja wa Emirates tangu mwezi Januaru mwaka huu baada ya jana usiku kuinyuka Arsenal bao 3-1.
Manchester United walipata bao la kwanza katika dakika ya 4 ya mchezo lililofungwa na Antonio Valencia na kuiweka kifua mbele timu yake kabla ya Jesse Lingard kufunga la pili dakika ya 11 baada ya kumkoonya mpira Shkodran Mustafi.
Kikosi cha Jose Mourinho kilipunguzwa na kuwa na wachezaji 10 katika dakika za mwisho baada ya Paul Pogba kupewa kadi nyekundu kwa kucheza rafu.
Kabla ya Pogba kupewa kadi nyekundi alimshinda nguvu Koscielny na kumpatia pasi Lingaard ambaye alifunga bao la tatu dakika ya 63 na kuipatia United ushindi huo.
Bao la kufutia machozi la Arsenal lilifungwa na Alexandre Lacazette katika dakika ya 49
Kipa wa United, David de Gea ameisaidia timu yake katika mechi yote.
Katika michezo mingine iliyofanyika jana Chelsea ikiwa nyumbani imeiadhibu Newcastle United bao 3-1, wakati Brighton ikipokea kichapo cha bao 5-1 kutoka kwa Liverpool.
Nayo Everton imeutumia vizuri uwanja wake wa nyumbani baada ya kushinda bao 2-0 dhidi ya Huddersfield huku Leicester ikipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Burnley.
Michezo mingine Stoke 2 Swansea 1, Watford 1 Tottenham 1, West Brom 0 Crystal Palace 0.
TAG