TIMU ZA SPAIN ZAISAPOTI BARCELONA KUWAOMBEA WAHANGA WA SHAMBULIO.

 Barcelona wakitulia kwa muda kuwaombea wahanga.


Wachezaji wa Barcelona na benchi lao la Ufundi, leo walilazimika kusimama kimya kwa dakika moja kabla ya mazoezi yao ili kuwafariji watu waliokufa katika milipuko ya kigaidi mjini humo.

Mashambulio mawili ya gari mjini Barcelona nja ukanda ewa bahari mjini Cambrils Alhamisi na mapema Ijumaa asubuhi yamechukua uhai wa watu 14, huku wengine wapatao 130 wakijeruhiwa. 

Polisi wamewapiga risasi na kuwaua watu watano waliojivalisha mabomu feki baada ya shambulio la Cambrils, wakati dereva wa basi dogo lililotumika kwenye shambulio la Barcelona bado hajapatikana. 


Real Madrid wakitulia kwa muda kuwaombea wahanga.

Mapema tu Barca ilithibitisha wachezaji wake watafunga vitambaa vyeusi mikononi kwenye mchezo wao wa ufunguzi wa msimu mpya wa La Liga dhidi ya Real Betis Uwanja wa Nou Camp Jumapili.

Real Madrid nao walitulia kwa dakika moja kabla ya kuanza mazoezi ya Ijumaa, kufuatia mashambulio mawili ya kigaidi nchini Hispania.

Real wanatarajiwa kuanza kampeni ya kutetea taji lao Ligi Kuu ya Hispania, maarufu kama La Liga ugenini dhidi ya Deportivo La Coruna Jumapili




Wakati huo huo: Kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola ambaye kwa sasa anafundisha Manchester City naye ametoa pole kwa tukio hilo.
TAG