BUNDESLIGA YAANZA KASI YAKE, BUYERN YAANZA KUTETEA KOMBE LAKE.


Bundesliga imeanza  kutimua  vumbi  siku  ya  Ijumaa tarehe  18  kwa  pambano  kati  ya  mabingwa  watetezi Bayern  Munich  na  Bayer  Leverkusen  katika  uwanja  wa Allianz  Arena. Lakini  nini  kinachotarajiwa  mara  hii  katika msimu  huu  wa  55  wa  Bundesliga, ambapo  timu zinazoonekana  kuwa  na  utamaduni  wa  kushika  nafasi za  juu  kama  Schalke 04, Bayer Leverkusen , Borussia Moenchengladbach  zimeporomoka  na  hata  hazimo katika  mashindano  ya  ligi  ya  Europa, mara  hii.
Fußball Bundesliga Ousmane Dembele FC Schalke 04 - Borussia Dortmund (picture-alliance/Sport Moments/Paschertz)
Ousmane Dembele wa Borussia Dortmund anataka kuhamia FC Barcelona
Kwa  upande  wa  tetesi  za  kuhama  wachezaji , tetesi kumhusu Ousmane  Dembele  wa  Borussia  Dortmund hazija muacha  salama. Kila  siku  tetsi  hizo  zinazidi kuongezeka  akihusishwa  na  kuhamia  FC  Barcelona  ya Uhispania.  Dembele  kutokana  na  utovu  wa  nidhamu ambapo  alishindwa  kufika  katika  mazowezi  ya  timu hiyo  siku  ya  Alhamis ameadhibiwa  kwa  kuondolewa katika  kikosi  cha  kwanza  na  atakaa  nje  ya  kikosi  hicho hadi  mwishoni  mwa  mwezi  huu.
Dembele  amefanya hivyo  akitaka  kutoa  mbinyo  kwa  timu  yake  kumruhusu kwenda  kuchezea  Barcelona. Barcelona  wametoa  kiasi cha  euro milioni 90  pamoja  na  malipo  mengine  ya bonasi  hapo  baadae  kuweza  kumpata  mchezaji  huyo chipukizi  mwenye umri  wa  miaka  20, raia  wa  Ufaransa. Lakini  Dortmund  wamekataa  wakitaka  kitita  cha  euro milioni 140  hadi 150  ili  kuweza  kumuachia  mchezaji huyo.
Rot-Weiss Essen v. Borussia Dortmund Ousmane Dembele (Bongarts/Getty Images)
Mchezaji wa kiungo wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele
Barcelona yatakiwa kusajili wachezaji wapya
Barcelona inalazimika  kusajili  wachezaji  wapya , amesema  mchezaji  wa  kiungo  wa  timu  hiyo Sergio Busquets , na  timu  hiyo  inawania  kuwasajili  Ousmane Dembele  wa  Borussia  Dortmund  na Philippe Coutinho wa  Liverpool  ili  kuimarisha  kikosi  chake  kilichoondokewa na  mchezaji  nyota  Neymar  ambaye  ametimkia Paris St. Germain  kwa  kitita  cha  milioni  222.
TAG